Soma magazeti ya leo kupitia KIDS GENERATION TANZANIA.
Contact Form 0742667518
July 25, 2018
Kila baada ya sekunde saba msichana Mwenye umri chini ya miaka 18 huozeshwa
Ripoti mpya ya shirika la Save the Children ya 2016 inasema msichana wa chini ya miaka 15 huozwa kila baada ya sekunde saba duniani.
Ripoti hiyo inasema watoto wa hadi chini ya miaka 10 wanashurutishwa kuolewa na wanaume wazee katika nchi kama vile Afghanistan, Yemen, India na Somalia.
Save the Children wanasema ndoa za mapema zinaweza kuchangia msururu wa matatizo ambayo huathiri maisha yote ya msichana.
Mizozo, umaskini na migogoro ya kibinadamu vinatazamwa kama sababu kuu zinazowaweka wasichana hatarini ya kuozwa wakiwa bado wana umri mdogo.
Subscribe to:
Posts (Atom)











