Contact Form 0742667518

Name

Email *

Message *

August 28, 2018

WATOTO NA VIPAJI.
Msichana kutoka Githurai nchini Kenya, Gracious Amani ‘Amani G’ aliyemkuna Staa wa muziki kutoka Marekani, Alicia Keys kwa uwezo wake wa kuimba wimbo wa ‘ Girl On Fire’,Julai 17 2018 aliingia Location na Director wa video za muziki wa nchini humo, Young Wallace.
Msichana huyo anayesoma Darasa la Nane katika shule ya msingi Githurai nchini humo, tayari alishatangazwa kuwa atatumia jina la sanaa kama ‘Amani G’ na kwa sasa anafanya kazi zake za muziki chini ya lebo ya muziki ya Pine Greek Records  iliyoko Nairobi nchini humo inayomilikiwa na Peter Nduati.

#NEW_GENERATION_WITH_CHANGES
KIDS GENERATION


#Watoto na vipaji
Sheila Sheldon ana umri wa miaka 9 pekee lakini uchoraji wake ni wa kiwango cha juu ikilinganishwa na watoto wa rika lake.

Yeye huchora picha ili kujifurahisha lakini cha kushangaza ni kwamba licha ya kuanza uchoraji akiwa na umri wa miaka sita hajapata mafunzo yoyote ya uchoraji.


Na tayari ameanza kugonga vichwa vya habari baada ya kuchora picha ya Rais Uhuru Kenyatta na kuvutia mwaliko katika ikulu ya rais huyo wa Kenya.

Vile vile amewahi kuchora picha za Gavana wa Mombasa Hassan Joho, Gavana wa Kwale Salim Mvurya na mbunge wa Mvita Abdulswamad Nassir.

Kipaji cha uchoraji wake kwanza kiligunduliwa katika shule ya kimataifa ya Diani International School.