Ripoti mpya ya shirika la Save the Children ta mwaka 2016 inasema msichana wa chini ya miaka 15 huozwa kila baada ya sekunde saba duniani.
Ripoti hiyo inasema watoto wa hadi chini ya miaka 10 wanashurutishwa kuolewa na wanaume wazee katika nchi kama vile Afghanistan, Yemen, India na Somalia.
Save the Children wanasema ndoa za mapema zinaweza kuchangia msururu wa matatizo ambayo huathiri maisha yote ya msichana.
Mizozo, umaskini na migogoro ya kibinadamu vinatazamwa kama sababu kuu zinazowaweka wasichana hatarini ya kuozwa wakiwa bado wana umri mdogo.